Treni ya Uthibitisho: #KIKAOCHA MAZUNGUMZO 27 APRILI. TAFADHALI SEMA kwenye KingsChat Web
Devotional
SEMA UKWELI KATIKA MOYO WAKO NA MHUBIRI CHRIS OYAKHILOME
BWANA, ni nani atakayekaa katika hema yako? ni nani atakayekaa katika mlima wako mtakatifu? Ni yeye aendaye kwa unyofu, na atendeaye haki, na asemaye kweli moyoni mwake (Zaburi 15:1-2).
Ikiwa unataka kutembea katika utukufu wa Mungu na kuwa na neema na nguvu zake zikiwadhihirishwa katika maisha yako, Neno linasema lazima utembee kwa unyofu, ufanye haki, na useme kweli moyoni mwako. Sasa, inamaanisha nini kusema kweli moyoni mwako? Hapa ndipo watu wengi hukosea. Hawana tatizo kutembea kwa unyofu; hawana tatizo kufanya haki, yaani, kufanya lililo sawa, lakini wanapata shida na "kusema kweli moyoni mwao."
Angalia kwamba mtunga zaburi hakusema, "Yeye... asemaye kweli kwa jirani yake"; hapana! Najua tafsiri chache zinaeleza kwa njia ambayo inaonekana kupendekeza kwamba inapaswa kusomeka "kusema kweli kwa mtu mwingine," lakini unapojifunza kutoka kwa tafsiri ya Kiebrania ya asili, utaona haina uhusiano wowote na kuzungumza na mtu mwingine. Toleo la Amplified linaeleza wazi: "Yeye atembeaye kwa uadilifu na nguvu ya tabia, na atendeaye haki, Na asemaye na kushikilia kweli moyoni mwake."
Je, umeona hilo? Inahusu kusema na kushikilia kweli moyoni mwako, na hiyo inamaanisha nini? Inamaanisha kutafakari: kusema na kufikiri kweli moyoni mwako. Hiyo ni kutafakari juu ya Neno la Mungu. Ikiwa unataka kutembea katika utukufu na upako wa Roho; ikiwa unataka kuona nguvu za Mungu zikidhihirishwa katika roho yako na katika maisha yako, lazima useme Neno. Lazima utoe nafasi na kutoa maelezo kwa Neno. Neno la Mungu katika kinywa chako ni Mungu akiongea; ni nguvu inayoshinda ambayo haiwezi kuzuiwa.
1 Timotheo 4:15 inasema kutafakari na kujitoa kabisa kwa Neno; shikilia kweli ya Neno la Mungu moyoni mwako; usiiache. Kataa kuyumbishwa na hali, na mafanikio yako, ushindi, maendeleo na ustawi vitakuwa dhahiri bila shaka, na visivyoweza kuzuilika.
MAOMBI
Baba mpendwa, asante kwa Neno lako liko moyoni mwangu na kinywani mwangu. Ninapotafakari na kutoa sauti, ninapata maendeleo, kupandishwa cheo, upanuzi, na kuenea kila upande. Niko katika safari ya juu na mbele tu. Utukufu wako, neema, na nguvu zako zinadhihirishwa katika maisha yangu na katika yote nifanyayo, kwa Jina la Yesu. Amina.
Salvation Prayer
O Lord God, I believe with all my heart in Jesus Christ, Son of the living God. I believe He died for me and God raised Him from the dead. I believe He's alive today.
I confess with my mouth that Jesus Christ is the Lord of my life from this day. Through Him and in His Name, I have eternal life; I'm born again.
Thank you Lord, for saving my soul! I'm now a child of God. Hallelujah!