Treni ya Uthibitisho: #KIKAOCHAKUZUNGUMZA TAFADHALI SEMA MANENO HAYA kwenye KingsChat Web
Devotional
ISHI KWA FURAHA NA SHANGWE KILA SIKU NA MHUBIRI CHRIS OYAKHILOME.
Ambaye ingawa hamjamwona, mnapenda; ambaye ingawa sasa hamuoni, lakini mnaamini, mnashangilia kwa furaha isiyoweza kusemwa na yenye utukufu (1 Petro 1:8).
Unapaswa kuishi kwa furaha kila siku, na furaha yako na shangwe yako inapaswa kuwa huru na hali. Hakuna kitu, na hakuna mtu, aliyeumbwa ili kukufanya uwe na furaha; wewe ndiye unayehusika na furaha na shangwe yako. Kamwe usijikute ukiwa na huzuni, na kuchanganyikiwa. Kamwe usiendelee na siku ukiwa na mtazamo wa kutoridhika na wasiwasi. Kuchanganyikiwa na unyogovu ni kazi za shetani.
Kamwe usiruhusu hayo maishani mwako. Badala yake, kila wakati ruhusu furaha ya Bwana ijaze moyo wako. Uwe na furaha kila wakati! Katika Yohana 15:11, Yesu alisema, "Haya nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu iwe timilifu." Tamaa yake ni wewe uwe na furaha saa ishirini na nne kwa siku, bila kujali hali unazokabiliana nazo. Hataki uwe na wasiwasi juu ya chochote.
Watu wengine wanapenda kuwa na wasiwasi. Wanadhani kuwa na wasiwasi ni ishara ya kuwajibika. Wanawasiwasi kuhusu ada za shule za watoto, wanawasiwasi kuhusu kazi yao, wanawasiwasi kuhusu hali ya afya yao, wanawasiwasi kuhusu wenzi wao, na wanawasiwasi kuhusu mambo mengi. Hiyo siyo maisha ya Mkristo.
Mkristo ameletwa katika maisha ya pumziko, yaliyojaa furaha na utukufu. Wafilipi 4:4 inasema, "Furahini katika Bwana siku zote; tena nasema, Furahini." Hata unapokabiliwa na changamoto, unapaswa kufurahi! Hakusema unapaswa kufurahi tu wakati kila kitu kiko sawa; hapana. Alisema, "Furahini katika Bwana siku zote." Kama usingeweza kufurahi kila wakati, Mungu asingekuambia ufanye hivyo. Ni kawaida kuhisi huzuni wakati mambo hayaonekani kuwa sawa; lakini ni hekima ya Mungu kufurahi hata katikati ya matatizo.
Usiruhusu chochote kikulemee. Fanya kile Neno linasema: Mtwikeni Bwana fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana na mambo yenu (1 Petro 5:7). Iwe shida iko katika fedha zako, afya, familia, masomo, chochote kile, mtwike Yeye, na furahi. Kisha, tamka kama Daudi, "Bwana ndiye mchungaji wangu; sitapungukiwa na kitu" (Zaburi 23:1). Katika uso wa changamoto au hali zisizopendeza, badala ya kujiuliza nini cha kufanya na tatizo ni nini, cheka! Cheka na cheka! Furahi katika Roho Mtakatifu, ukijua kuwa furaha ya Bwana ni nguvu yako. Halleluya!
Salvation Prayer
O Lord God, I believe with all my heart in Jesus Christ, Son of the living God. I believe He died for me and God raised Him from the dead. I believe He's alive today.
I confess with my mouth that Jesus Christ is the Lord of my life from this day. Through Him and in His Name, I have eternal life; I'm born again.
Thank you Lord, for saving my soul! I'm now a child of God. Hallelujah!