Imani ya Leo: #RHEMAFORTODAY 1 JULAI. Sema haya kwenye KingsChat Web
Devotional
AMANA TAKATIFU ~ PASTOR CHRIS OYAKHILOME.
Kulingana na injili tukufu ya Mungu aliye barikiwa, ambayo ilikabidhiwa kwangu (1 Timotheo 1:11).
Mtume Paulo alichukua jukumu binafsi kwa Injili. Maneno yake katika mstari wetu wa mada yanaonyesha kwamba kwake, Injili ilikuwa amana takatifu. Katika 1 Wakorintho 9:16, alisema, "...nimewekewa sharti; naam, ole wangu, nisipoihubiri injili!" Tena, katika 1 Timotheo 1:12, alitangaza, "...namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu, kwa kuwa aliniona kuwa mwaminifu, akaniweka katika huduma.
Imani yako kuhusu Injili lazima iwe kamilifu. Fikiria hili: wokovu wa roho zilizopotea ni shauku kuu ya Mungu; ni yote ambayo mbingu inasimamia. Hata hivyo, Mungu alikabidhi agizo na jukumu kubwa kama hili kwako na kwangu. Hili ni jambo la kuheshimiwa; ni takatifu sana kuchukulia kwa wepesi.
Katika Marko 16:15, Yesu alisema, "...Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri injili kwa kila kiumbe"; hili ni Agizo Kuu. Swali ni, "Je, Mungu anaweza kukuamini kutimiza hilo? Je, uko katika biashara yake, au bado unashughulika na ndoto zako mwenyewe? Acha Injili, na uenezaji wake duniani kote, iwe na maana zaidi kwako kuliko kitu kingine chochote katika ulimwengu huu. Jitolee kwa hilo, bila kujali upinzani unaoweza kukumbana nao.
Chukua mfano kutoka kwa Paulo; hata wakati Roho Mtakatifu alishuhudia wazi kwamba angekumbana na mateso makali na kufungwa ikiwa angeenda kuhubiri huko Yerusalemu (Matendo 20:22-23), hakuogopa. Jibu lake lilikuwa: "... hakuna hata moja ya mambo haya yanayonisumbua, wala sihesabu maisha yangu kuwa ya thamani kwangu, ili niweze kumaliza mwendo wangu kwa furaha, na huduma, niliyopokea kutoka kwa Bwana Yesu, kushuhudia injili ya neema ya Mungu" (Matendo 20:24). Kuzungumzia kuchoma madaraja yako? Hicho ndicho!
Kuwa mwanaharakati wa Injili. Hakuna shida unazokumbana nazo zinazoweza kukushinda ikiwa utasimama imara na kukataa kukata tamaa. Kumbuka kwamba Mungu alikuona mwaminifu na kukabidhi Injili kwako; Anaamini ndani yako. Kwa hivyo, kuwa shahidi mzuri wa Bwana Yesu Kristo, na ufanye hivyo kwa shauku na furaha. Hallelujah!
MAOMBI
Baba mpendwa, Neno lako na Roho Mtakatifu hunijaza ujasiri na nguvu ya kuhubiri Injili, na ninafanya hivyo kwa furaha kama shahidi mzuri wa Yesu Kristo. Asante kwa utimilifu usio na kifani ninaoupata ninaposhinda roho na kuwaongoza wengi kwenye haki, katika Jina la Yesu. Amina.
Salvation Prayer
O Lord God, I believe with all my heart in Jesus Christ, Son of the living God. I believe He died for me and God raised Him from the dead. I believe He's alive today.
I confess with my mouth that Jesus Christ is the Lord of my life from this day. Through Him and in His Name, I have eternal life; I'm born again.
Thank you Lord, for saving my soul! I'm now a child of God. Hallelujah!